Author Archives: Dr. Makirita Amani

About Dr. Makirita Amani

Dr. Makirita Amani ni daktari wa binadamu, mwandishi, mhamasishaji na mjasiriamali. Dhumuni lake kubwa kwenye maisha ni KUWASAIDA WATU KUBORESHA MAISHA YAO NA KUFIKIA MAFANIKIO MAKUBWA KUPITIA KAZI ANAZOFANYA. Mawasiliano 0717396253 email makirita@kisimachamaarifa.co.tz

3216; Fokasi, Muda Na Msimamo.

By | October 21, 2023

3216; Fokasi, Muda Na Msimamo. Rafiki yangu mpendwa,Kila kitu kinafanya kazi,Kila biashara inalipa,Kila kazi inaweza kukupa chochote unachotaka.Lakini bado tunaona watu wanahangaika na mambo mengi na hawapati kile wanachotaka. Siyo kwamba watu hao hawajui wanachotaka, wanakuwa wanajua sana.Siyo kwamba wanakuwa hawajui wanachopaswa kufanya, wanakijua sana.Na wakati mwingine siyo kwamba ni (more…)

3215; Maswali na ngazi zake.

By | October 20, 2023

3215; Maswali na ngazi zake. Rafiki yangu mpendwa,Unaweza kuijua ngazi ambayo mtu amefikia kwenye safari yake ya mafanikio kupitia maswali anayokuwa anauliza kuhusu kile anachofanya au kutaka kufanya. Wachanga kabisa huwa wanauliza maswali ya NINI.Swali kuu likiwa NINI wafanye kwenye hatua fulani waliyopo au ili kupiga hatua fulani.Hii ni ngazi (more…)

3214; Kupoteza kabla ya kupata.

By | October 19, 2023

3214; Kupoteza kabla ya kupata. Rafiki yangu mpendwa,Kufanya biashara na ujasiriamali ni sawa na kucheza mchezo ambao unaanza kwa kupoteza kabla ya kupata.Na hilo ndiyo limekuwa linawakwamisha wengi wanaoanza wasiendelee. Unapoianza safari, unaanza kwa kupoteza muda.Hapa unajikuta ukitumia muda wako mwingi kwenye kujenga biashara ambayo una ndoto nayo itakuja kuwa (more…)

3213; Aibu.

By | October 18, 2023

3213; Aibu. Rafiki yangu mpendwa,Bilionea Peter Thiel amewahi kunukuliwa akisema watu wengi walioweza kuanzisha makampuni yaliyoleta mapinduzi makubwa hapa duniani, walikuwa na ugonjwa fulani wa akili ambapo hawajali wengine wanawachukuliaje.Pale watu hao wanapoamua kitu cha kufanya, wanakifanya kama walivyopanga bila ya kukubali kukwamishwa na kitu chochote. Katika kulijadili hilo, swali (more…)

3212; Epuka kujidanganya mwenyewe.

By | October 17, 2023

3212; Epuka kujidanganya mwenyewe. Rafiki yangu mpendwa,Mwanafizikia Richard Feynman amewahi kunukuliwa akisema wajibu wako wa kwanza kwenye maisha ni kuhakikisha hujidanganyi, kwa sababu ni rahisi sana mtu kujidanganya mwenyewe. Mtu unaweza kuchukulia kauli hiyo kirahisi na kuona huwezi kujidanganya, kwani unajiambia ukweli mara zote.Lakini huo huo ukweli unaodhani unajiambia, ndiyo (more…)

3211; Ukiacha kukwepa.

By | October 16, 2023

3211; Ukiacha kukwepa. Rafiki yangu mpendwa,Ni jambo la kushangaza, lakini kuna mambo unayojua unapaswa uyafanye, lakini umekuwa unayakwepa.Mambo hayo ndiyo yenye nguvu ya kukufikisha kule unakotaka kufika. Na katika mambo mengi unayopaswa kuyafanya, kuna moja muhimu sana ambalo lina nguvu ya kuleta matokeo makubwa na ya tofauti.Hilo nalo umekuwa hulipi (more…)

3210; Mkokoteni mbele ya punda.

By | October 15, 2023

3210; Mkokoteni mbele ya punda. Rafiki yangu mpendwa,Pata picha kuna mtu umempa kazi ya kubeba mizigo kutoka sehemu moja kwenda nyingine.Amatakiwa kutumia mkokoteni na punda.Unamwelekeza mtu huyo, pakia mzigo kwenye huo mkokoteni, kisha ufunge kwenye punda na uupeleke.Unaondoka ukiwa umemwachia maagizo hayo.Anakupigia simu kwamba amefuata maelekezo lakini mzigo haujaweza kwenda.Unamuuliza (more…)

3209; Ngumu kutunza kuliko kutengeneza.

By | October 14, 2023

3209; Ngumu kutunza kuliko kutengeneza. Rafiki yangu mpendwa,Unapokuwa unaanzia chini kabisa, kiu yako kubwa inakuwa ni kufanikiwa na kufika juu.Unakuwa tayari kufanya kila kinachopaswa kufanyika ili upate matokeo unayoyataka.Safari inaweza kuwa ngumu, lakini kwa sababu ya kujitoa kweli kweli, unafika ulikokuwa unataka kufika. Hapo sasa ndipo penye hatari kubwa sana (more…)

3208; Unajua lakini hufanyi.

By | October 13, 2023

3208; Unajua lakini hufanyi. Rafiki yangu mpendwa, Kwenye ukurasa uliopita wa 3207 tumejifunza umuhimu wa kuchukua hatua ili kuzalisha matokeo tunayotaka badala ya kusubiri matokeo yajizalishe yenyewe. Hilo ni jambo ambalo kila anayetaka mafanikio makubwa analijua, kwamba matokeo makubwa hayatokei tu, bali yanasababishwa. Tukiendelea na mfano wa ukurasa huo, kwenye (more…)

3207; Simu ziite sasa.

By | October 12, 2023

3207; Simu ziite sasa. Rafiki yangu mpendwa,Nimekuwa naona watu wakiweka picha za bidhaa mbalimbali wanazouza kwenye mtandao (wasap status) pamoja na bei zake.Kisha wanaweka maelezo; simu ziite sasa.Nimekuwa nachukulia kauli hiyo kama utani tu na kuona hakuna muuzaji aliye makini anayekuwa anategemea kweli kwamba simu zitaita. Siku moja nilikuwa namfanyia (more…)