Author Archives: Dr. Makirita Amani

About Dr. Makirita Amani

Dr. Makirita Amani ni daktari wa binadamu, mwandishi, mhamasishaji na mjasiriamali. Dhumuni lake kubwa kwenye maisha ni KUWASAIDA WATU KUBORESHA MAISHA YAO NA KUFIKIA MAFANIKIO MAKUBWA KUPITIA KAZI ANAZOFANYA. Mawasiliano 0717396253 email makirita@kisimachamaarifa.co.tz

Barua ya XXI; Kuhusu Sifa ambazo falsafa ya Ustoa inatupatia.

By | September 22, 2023

Barua ya XXI; Kuhusu Sifa ambazo falsafa ya Ustoa inatupatia. Rafiki yangu Mstoa, Sisi binadamu huwa tunapenda kuwa na sifa fulani mbele ya wengine.Huwa tunapenda umaarufu kupitia yale tunayofanya au tunayokuwa nayo kwenye maisha.Na tamaa hiyo ya sifa na umaarufu ndiyo inawasukuma wengi kufanya hata mambo yasiyo sahihi ili tu (more…)

3187; Siyo ngumu kihivyo.

By | September 22, 2023

3187; Siyo ngumu kihivyo. Rafiki yangu mpendwa,Watu wengi wamekuwa wanalalamika maisha ni magumu na kuna ukweli fulani kwenye hilo.Lakini bado tukiangalia kwenye uhalisia, maisha siyo magumu kihivyo, bali watu wenyewe wamekuwa wanazidisha ugumu wa maisha kwa mambo wanayofanya. Kwa mfano kwa walio wengi, kuamka asubuhi na mapema ili kuianza siku (more…)

3186; Mrejesho wa watu.

By | September 21, 2023

3186; Mrejesho wa watu. Rafiki yangu mpendwa,Sisi binadamu kama viumbe wa kijamii, huwa tunapenda sana kuwa ndani ya kundi la watu.Ili kujihakikishia nafasi yetu kwenye kundi lolote tulilopo, huwa tunajali sana kuhusu mrejesho wa watu wengine kuhusu sisi. Huwa tunataka sana kukubalika na kila mtu, tukiamini ndiyo njia salama ya (more…)

3185; Mateso unayoyafurahia.

By | September 20, 2023

3185; Mateso unayoyafurahia. Rafiki yangu mpendwa,Huwa kuna kauli inayosema watu waliofanikiwa wanakuwa wamefanya vitu ambavyo wasiofanikiwa hawapendi kuvifanya. Pia ni vitu ambavyo wao wenyewe hawapendi kuvifanya, ila wanakuwa hawana namna bali kuvifanya. Ukweli ni kwamba huwezi kupata mafanikio makubwa kwa kufanya yale ambayo kila mtu anayafanya, tena kwa namna ambavyo (more…)

3184; Haina Mjadala.

By | September 19, 2023

3184; Haina Mjadala. Rafiki yangu mpendwa,Kwenye safari ya kujenga mafanikio makubwa kwenye maisha, lazima uwe na mchakato ambao unaufuata mara zote bila kuacha.Unapaswa kuwa na mambo ambayo utayafanya bila ya kuruhusu hofu au sababu zozote zile kukuzuia.Hii ni dhana inayoitwa Haina Mjadala (Non Negotiable). Kwenye mambo hayo, hupotezi muda kujiuliza (more…)

3183; Nini naweza kupenda kwake?

By | September 18, 2023

3183; Nini naweza kupenda kwake? Rafiki yangu mpendwa,Wateja tulionao kwenye kile tunachouza ni watu muhimu sana kwetu.Hao ndiyo wanaotuwezesha kulipa gharama mbalimbali kwenye maisha yetu. Ni kupitia wao kununua kwetu ndiyo tunapata fedha za kuyaendesha maisha yetu.Wateja wanaonunua kwetu ni watu muhimu sana kwetu. Swali ni je tunawafanyaje ili waweze (more…)

3182; Suuza kisha rudia.

By | September 17, 2023

3182; Suuza kisha rudia. Rafiki yangu mpendwa,Japokuwa safari ya kupata mafanikio makubwa kwenye maisha ni ngumu, watu wamekuwa wanazidisha ugumu huo kwa kuamua kuacha kufanya yale ya msingi kwenye hiyo safari. Kwenye kila eneo la maisha, huwa kuna mambo mengi ya kufanya.Lakini yapo ya msingi kabisa ambayo ni lazima yafanywe (more…)

3181; Tuko hapa kwa ajili ya utekelezaji.

By | September 16, 2023

3181; Tuko hapa kwa ajili ya utekelezaji. Rafiki yangu mpendwa,Kipindi cha nyuma, maarifa yalikuwa adimu sana kiasi cha watu kuwa tayari kuwa tayari kulipa gharama kubwa ili kuyapata na kuyatumia kupiga hatua kubwa.Kadhalika kwa mawazo mazuri ya biashara na miradi mingine.Kuna watu waliweza kuingiza kipato kikubwa kwa kuuza tu mawazo (more…)

Barua ya XX; Kuhusu kuishi yale unayohubiri.

By | September 15, 2023

Barua ya XX; Kuhusu kuishi yale unayohubiri. Rafiki yangu Mstoa,Kusema huwa ni rahisi sana, kila mtu ni msemaji mzuri. Lakini inapokuja kwenye kutenda, wengi siyo wazuri. Kushauri wengine pia ni rahisi sana, na wengi ni washauri wazuri. Lakini mara nyingi unakuta anayetoa ushauri ndiye anauhitaji zaidi huo ushauri anaotoa, ila (more…)

3180; Sitaki upate amani.

By | September 15, 2023

3180; Sitaki upate amani. Rafiki yangu mpendwa,Siku za karibuni nilikuwa nampigia mmoja wetu hapa simu.Akaniambia nikiona simu yako nakosa amani.Nikamwambia hivyo ni vizuri kabisa, kwa sababu hicho ni kiashiria kwamba programu inafanya kazi. Japokuwa jina langu ni Amani, hicho ndiyo kitu ambacho sitataka ukipate kabisa.Kwa sababu kupitia kujifunza kwa usomaji (more…)