Category Archives: KUTOKA KWA KOCHA

Hizi ni makala kwa wasomaji wote wa KISIMA CHA MAARIFA.

#TAFAKARI YA LEO; GUSA MAISHA YA WENGINE…

By | February 7, 2021

Ni rahisi kusema unatekeleza tu wajibu wako bila kujali nini kinatokea kwa wengine.Ni rahisi kujali maslahi yako bila ya kujali ya wengine. Inashawishi kupambana na hali yako na kuwaacha wengine wapambane na hali zao.Hayo yanaweza kukupa kile unachotaka, yanaweza kukufanya ubaki kwenye kazi yako, lakini hayatakufanya uache alama yoyote.Hakuna anayekumbukwa (more…)

#TAFAKARI YA LEO; FANYA KAMA UNAMSHAURI MWINGINE…

By | February 6, 2021

Inapokuja kwenye matatizo ya wengine, ni rahisi sana kuwashauri, huwa hatukuso chochote cha kuwaambia. Lakini inapokuja kwenye matatizo yetu wenyewe, tunajikuta tumekwama na hatujui nini cha kufanya. Hiyo ni kwa sababu tunakuwa tumeweka hisia zaidi kwenye matatizo yetu na hisia zinapokuwa juu, fikra zinakuwa chini. Unapokuwa kwenye matatizo yoyote yale, (more…)

#TAFAKARI YA LEO; NJIA YA KUZISHINDA MASHINE…

By | February 5, 2021

Mashine ya kwanza ya kushona nguo iliharibiwa vibaya na watu kwa sababu waliamini ni adui kwa ajira zao. Tangu kuanza kwa ugunduzi wa mashine za kurahisisha kazi, watu wamekuwa wanazihofia na kuzipinga, kwa sababu ni adui anayechukua ajira nyingi. Lakini kwa zama hizi hatuwezi tena vita hiyo, mashine zimeshakuwa sehemu (more…)

#TAFAKARI YA LEO; TATIZO LA MBIO ZA PANYA…

By | February 4, 2021

Watu huwa wanajaribu kukuweka kwenye mashindano ya kila aina. Na ndani yetu binadamu, huwa tuna roho ya kupenda kushindana. Ila tatizo kubwa la mashindano hayo ni hata ukishinda, hakuna unachonufaika nacho. Unaweza kubishana na watu na ukawashinda, lakini hutakuwa umewabadili. Unaweza kushindana kibiashara na kuona umeshinda, lakini kiuhalisia hujashinda. Tatizo (more…)

#TAFAKARI YA LEO; ANGALIA MASLAHI YAO…

By | February 3, 2021

Watu wanaweza kufanya vitu ambavyo vinatushangaza, tukashindwa kuelewa kwa nini wamefanya hivyo. Ipo njia rahisi ya kuwaelewa watu kwa yale wanayofanya, ambayo ni kuangalia maslahi yao kwenye kile wanachofanya. Kwa asili sisi binadamu ni wabinafsi, tunatanguliza maslahi yetu mbele kabla ya kingine chochote. Hivyo unapomuona mtu anafanya kitu, hata kama (more…)

#TAFAKARI YA LEO; JE NI UKWELI?

By | February 2, 2021

Hili ni swali la kwanza na muhimu kabisa kujiuliza kwenye jambo lolote lile. Ni rahisi sana kuamini yale ambayo watu wanatuambia hasa wanapoonekana kusema kutoka ndani ya mioyo yao na kwa ushawishi. Tunachosahau ni kwamba kila mtu huwa anadanganya, wapo wanaofanya hivyo kwa kujua, ambao hawa hufanya hivyo kulinda maslahi (more…)

#TAFAKARI YA LEO; UWEZO WA KUFIKIRI NDIYO CHANZO CHA MAKUBWA…

By | February 1, 2021

Uwezo wetu wanafamu wa kufikiri, ndiyo chanzo cha maendeleo yote duniani. Kila unachokiona kwa macho yako leo, kilianza kama fikra kwenye akili ya mtu. Na hazikuwa fikra za kawaida, kabla ya vitu hivyo kuwepo, wengi waliamini haviwezekani. Wale waliofikiri vitu hivyo, walionekana kama wamechanganyikiwa au wanaota tu. Lakini hawakukata tamaa, (more…)

#TAFAKARI YA LEO; UONGO NDIYO MSINGI WA MAOVU…

By | January 31, 2021

Kila uovu unaofanyika, huwa unaanzia kwenye uongo. Tena uongo unaanza kidogo, lakini unaendelea kukua ili kulinda uongo wa mwanzo. Lakini pia mtu anapotumia uongo na ukamfanikishia kile anachotaka, anashawishika zaidi kuendelea na uovu mwingine. Wengi huanza na uongo kidogo, wakijiambia hawataendelea hivyo, lakini uongo huo unapowapa wanachotaka, wanajikuta wakiendelea nao (more…)

#TAFAKARI YA LEO; UKWELI UNAHITAJI USHAHIDI…

By | January 30, 2021

Ukweli unahitaji ushahidi halisi, unaoonekana na kuweza kupimika na kila mtu. Ukweli unapaswa kuwa kweli kwa kila mtu na kila mahali. Ukweli ambao mtu analazimishwa kuamini bila ya ushahidi siyo ukweli huo. Kabla ya kukua kwa sayansi, watu waliamini mambo mengi ambayo siyo kweli. Dini na ushirikina viliwaweka watu kwenye (more…)

#TAFAKARI YA LEO; MUDA NI TIBA ISIYOSHINDWA…

By | January 29, 2021

Unaweza kuhangaika na jambo, ukaweka kila aina ya juhudi lakini bado usipate matokeo unayotaka. Hapo unapaswa kuuachia muda ufanye yake, kwa sababu muda ni tiba isiyoshindwa. Baada ya muda mrefu, suluhisho litajitokeza lenyewe au jambo unalohangaika nalo litapotea au kukosa umuhimu. Usijiumize au kukata tamaa pale juhudi unazoweka hazileti matokeo (more…)