Category Archives: KUTOKA KWA KOCHA

Hizi ni makala kwa wasomaji wote wa KISIMA CHA MAARIFA.

#TAFAKARI YA LEO; MATOKEO HAYAHALALISHI NJIA…

By | January 28, 2021

Watu wamekuwa wanatumia njia zisizo sahihi ili tu kupata matokeo wanayoyataka. Wakiamini kilicho muhimu ni matokeo na siyo njia iliyoleta matokeo hayo. Wanaamini matokeo yakiwa mazuri basi njia itakuwa sahihi. Lakini hilo siyo kweli, tumeona wengi wakianguka baada ya kupata matokeo waliyotaka kwa sababu njia walizotumia hazikuwa sahihi. Hakikisha unaanza (more…)

#TAFAKARI YA LEO; WASHA MSHUMAA…

By | January 27, 2021

Kama kuna giza, kitu chenye manufaa unachoweza kufanya ni kuwasha mshumaa. Usihangaike kulaumu au kulaani giza, hilo halitabadili chochote. Lakini kwa kuwasha mshumaa, unaleta mwanga ambao unaliondoa giza. Kuna maeneo mengi yenye giza kwenye maisha yako na ya wengine, angalia ni mshumaa upi unaoweza kuwasha kisha fanya hivyo. Kuwa chanzo (more…)

#TAFAKARI YA LEO; ZIADA, UHABA NA KIASI…

By | January 26, 2021

Ziada ni mbaya, chochote unachofanya au kuwa nacho kwa ziada huwa kinakulevya na kukupa kiburi. Unaona tayari umeshapata kila kitu. Uhaba nao ni mbaya, kwa sababu unachokosa unakihofia na kukuweka kwenye hali ya kutawaliwa na wale wanaoweza kukupatia unachokosa. Mpango mzima ni kuwa na kiasi, kufikia kiasi. Kwa kiasi, huna (more…)

#TAFAKARI YA LEO; FAIDA ISIYO SAHIHI NI HASARA…

By | January 25, 2021

Ipo kauli maarufu kwamba hakuna kipya chini ya jua, tungekuwa tunaielewa kauli hii, tungejiepusha na mengi. Lakini huwa hatuielewi, huwa hatujifunzi kwa historia na hivyo kurudia makosa yale yale. Angalia kwenye utapeli, hakujawahi kuja utapeli mpya kabisa, utapeli wowote ule unatumia uongo au tamaa kuwanasa watu. Hii ina maana kama (more…)

#TAFAKARI YA LEO; KWA NJE NI RAHISI…

By | January 24, 2021

Kitu chochote kile ukikiangalia kwa nje, huwa kinaonekana ni rahisi kufanya na chenye manufaa makubwa. Ni mpaka uingie ndani ndiyo unakua ugumu na changamoto za kitu hicho. Hali hii ya kuona vitu ni rahisi imekuwa kikwazo kwa wengi kupiga hatua kwa sababu unapokutana na ugumu kwenye kile ulichochagua kufanya, ni (more…)

#TAFAKARI YA LEO; FURAHIA UNAPOSHINDWA…

By | January 23, 2021

Unajifunza mengi unaposhindwa kuliko unaposhinda. Kushindwa kunakuonesha ni maeneo yapi una udhaifu, wapi bado hujawa vizuri na hivyo kulazimika kujifunza na kukazana uwe bora zaidi. Kushinda kunakufanya ujione uko vizuri, unajua kila kitu na hilo linapelekea uwe na kiburi kinachokupelekea kuanguka na kushindwa. Mara kwa mara jiweke kwenye mazingira ya (more…)

#TAFAKARI YA LEO; UNAPOAHIRISHA JAMBO…

By | January 22, 2021

Jambo lolote unalokuwa umejipangia kufanya halafu ukaliahirisha, maana yake ni kwamba umejiambia una jambo jingine muhimu zaidi la kufanya. Sasa hebu angalia mwenyewe, pale unapoahirisha jambo, ni nini unaenda kufanya? Mara nyingi unajikuta ukifanya mambo ya hovyo na yasiyo na tija kabisa. Badala ya kukamilisha kazi muhimu, unakimbilia kufuatilia habari (more…)

#TAFAKARI YA LEO; KUWA BORA ZAIDI YA JANA…

By | January 21, 2021

Ni rahisi kujipima na kushindana na wengine, lakini unapoingia tu kwenye mashindano hayo, unakuwa umejipoteza. Mtu sahihi wa kushindana naye ni wewe mwenyewe, kila siku kuhakikisha unakuwa bora kuliko ulivyokuwa jana yake. Wewe ndiye unayejijua zaidi, wewe ndiye unajua unataka nini na ndani yako una nini. Kama hujajua hayo, utahangaika (more…)

#TAFAKARI YA LEO; MADHARA YA FIKRA CHANYA.

By | January 20, 2021

Tumeshajifunza sana manufaa ya fikra chanya, namna zinavyotuwezesha kuziona fursa zaidi na kutupa matumaini badala ya kukata tamaa. Lakini kila lenye faida huwa pia lina hasara zake. Fikra chanya pia zina madhara kama haziambatani na matendo chanya. Kuna watu wanakuwa na fikra chanya kweli kweli, lakini hakuna hatua zozote chanya (more…)

#TAFAKARI YA LEO; BADILI MAZINGIRA…

By | January 19, 2021

Kama kuna tabia yoyote unayotaka kubadili kwenye maisha yako, anza kwa kubadili mazingira yako. Mazingira yana nguvu kubwa kwenye kujenga na kuimarisha tabia. Angalia ni mazingira yapi unakuwepo wakati wa tabia husika. Mfano kama unasumbuka na hasira, angalia ni wakati gani huwa unapata zaidi hasira, utagundua kuna vitu ukifanya au (more…)