Category Archives: KUTOKA KWA KOCHA

Hizi ni makala kwa wasomaji wote wa KISIMA CHA MAARIFA.

#TAFAKARI YA LEO; FURAHA SIYO RAHA MUDA WOTE…

By | January 18, 2021

Hadithi za utotoni zilikuwa zinamalizia na baada ya mateso wakaishi kwa raha mustarehe maisha yao yote. Hizo ni hadithi na siyo uhalisia. Hakuna maisha ya raha muda wote, kila wakati kuna ugumu au changamoto unakabiliana nayo na ukivuka inakuja nyingine. Furaha kwenye maisha ni kujua maana ya maisha yako, kujua (more…)

#TAFAKARI YA LEO; HESHIMU UNACHOJIFUNZA NA KUFANYA…

By | January 17, 2021

Kujifunza kitu mara moja haitoshi, unahitaji kurudia rudia. Kufanya kitu mara moja haikufikishi kwenye mafanikio makubwa, unapaswa kufanya mara kwa mara, kwa muda mrefu. Hapo ndipo inapokuja changamoto ya mazoea. Kwa sababu umekuwa unajifunza kitu kwa kurudia, unajiambia tayari unajua. Kwa sababu umekuwa unafanya kila siku, unajikuta ukifanya kwa mazoea. (more…)

#TAFAKARI YA LEO; KIKUTOKACHO KIPO NDANI YAKO…

By | January 16, 2021

Kama mtu amekukasirisha na kisha ukamtukana, tatizo siyo hasira ambayo umekuwa nayo, bali tatizo ni matusi yaliyo ndani yako. Huwezi kutoa kitu ambacho hakipo ndani yako. Kama hujui kuongea lugha ya kichina, hata ukasirishwe kiasi gani, hutaiongea, kwa sababu haipo ndani yako. Kwa mambo yote unayofanya au kusema na baadaye (more…)

#TAFAKARI YA LEO; KUJUA PEKEE HAITOSHI…

By | January 15, 2021

Hautafanikiwa na kuwa na maisha bora kwa sababu unajua vitu vingi. Bali utafanikiwa kwa kuweka kwenye matendo yale unayojua, hata kwa kiwango kidogo tu. Kujifunza kitu mara moja hakutoshi, unapaswa kurudia mara kwa mara mpaka kitu hicho kiwe sehemu yako, kiwe asili kwako. Chagua misingi utakayoendesha nayo maisha yako, iishi (more…)

#TAFAKARI YA LEO; HISIA NI KAMA MOTO…

By | January 14, 2021

Huwezi kufanya chochote bila hisia na huwezi kuwashawishi wengine bila kugusa hisia zao. Hisia ndiyo zinatoa msukumo kwa mtu kuchukua hatua fulani, lakini wengi wamekuwa wanazitumia kwa namna isiyo sahihi. Kwenye ukurasa wa 2205 unajifunza kwa kina namna sahihi ya kutumia hisia zako na za wengine, kwa namna ambayo zitaleta (more…)

#TAFAKARI YA LEO; NATAKA WEWE USHINDE…

By | January 13, 2021

Tunategemeana sana kwenye maisha, hakuna anayeweza kushinda peke yake. Ushindi wa mwalimu ni wanafunzi wanaofaulu, ushindi wa daktari ni wagonjwa wanaopona na ushindi wa mpishi ni watu wanaoshiba na kufurahia chakula. Chochote unachofanya, angalia wale unaowalenga wananufaikaje, wajibu wako ni kuhakikisha wanashinda, maana wakishinda hao, ndiyo na wewe unashinda pia. (more…)

#TAFAKARI YA LEO; FANYA CHOCHOTE…

By | January 12, 2021

Kama upo njia panda na hujui kipi cha kufanya, anza kufanya chochote. Kwa kufanya chochote ni rahisi kufika kwenye kilicho sahihi kwako kufanya kuliko kuendelea kusubiri. Kwa kuanza na chochote unajifunza na kupata msukuko wa kuendelea kuliko kusubiri. Unaweza kusubiri utakavyo, lakini tambua muda haukusubiri na muda ukishapita haurudi tena. (more…)

#TAFAKARI YA LEO; USIPOST UJINGA, FANYA KAZI…

By | January 11, 2021

Mitandao ya kijamii imewageuza watu kuwa misukule wanaofanya kazi bila kulipwa. Inawahadaa watu kwa umaarufu feki unaopatikana kwa kupost vitu vya kijinga mtandaoni. Lakini umaarufu huo hauna manufaa kwa mtu zaidi ya kumharibia sifa yake. Umaarufu wenye manufaa ni ule unaotokana na kazi inayotoa thamani kwa wengine, ila huo unahitaji (more…)

#TAFAKARI YA LEO; KUWA CHANYA KUNALIPA…

By | January 10, 2021

Katika kila jambo au hali unayopitia, kuwa chanya kunalipa kuliko kuwa hasi. Kuwa chanya kunakuonesha fursa zaidi wakati kuwa hasi kunakuonesha matatizo zaidi. Kuwa chanya kunakupa matumaini wakati kuwa hasi kunakukatisha tamaa. Pamoja na manufaa haya ya kuwa chanya, bado wengi hukimbilia kuwa hasi. Hiyo ni kwa sababu kuwa hasi (more…)

#TAFAKARI YA LEO; FANYA MAAMUZI YA MAISHA YAKO…

By | January 9, 2021

Watu wengi ni wazito kufanya maamuzi ya maisha yao. Hiyo ni kwa sababu kufanya maamuzi ni kugumu kuliko kufuata mkumbo. Wengi huishia kuangalia wengine wanafanya nini na kufanya pia, bila kujiuliza kama ndiyo kitu sahihi kwao kufanya. Wewe usiwe hivyo, usiruhusu maisha yako yaendeshwe na wengine kwa namna watakavyo. Fanya (more…)